MSICHANA Atu Gabriel mwenye umri wa
miaka 20 , mwanafunzi wa Chuo cha Eden
Hill kilichopo Kwamfipa wilayani Kibaha
mkoani Pwani, amekutwa amekufa chumbani
kwa mtu anayetajwa kuwa ni hawara yake,
Hafidh Mohammed .
Mwili wa Atu ukiwa chumbani kwa mtu
anayesadikika kuwa ni mpenzi wake, Hafidh
Mohammed.
Tukio hilo lilitokea April 26 , mwaka huu na
kukusanya umati huku mwanaume aliyelala
na binti huyo akitokomea
kusikojulikana.Marehemu anadaiwa kuwa
mwenyeji wa Makambako mkoani Njombe.
Akizungumza na waandishi wetu juzi Kibaha ,
mama wa Hafidh ambaye pia ni mjumbe wa
eneo hilo, Zainabu Saidi alisema mwanaye
alimweleza kutokea kwa tukio hilo asubuhi
kulipokucha na kabla ya hapo , hakuwa
akifahamu kama alikuwa na uhusiano wa
kimapenzi na msichana huyo kwa vile
aliyekuwa akimfahamu ni mwanamke
mwingine ambaye alizaa naye .
“Mimi kwa kweli sikuwa na taarifa yoyote juu
ya uhusiano wao na huyu mwanafunzi ,
nimeletewa taarifa asubuhi na kijana wangu
huku akionekana kuchanganyikiwa ,
nimejaribu kumsihi asikimbie lakini
imeshindikana,” alisema mama huyo.
Mwili wa Atu ukiingizwa kwenye gari la
polisi .
ALIVYOAGA CHUONI
Wanafunzi wa chuo hicho kinachofundisha
masomo ya biashara na habari ambao
walikataa kutaja majina yao waliliambia
gazeti hili kuwa , marehemu Atu aliwaaga
anakwenda jijini Dar es Salaam kumuuguza
wifi yake aliyelazwa katika Hospitali ya
Amana, Aprili 23, mwaka huu .
Hata hivyo , walisema uondokaji wake uliwapa
maswali mengi kwani tofauti na
walivyotegemea kuwa angebeba mfuko
mkubwa wenye nguo za kubadili , yeye
aliondoka akiwa na mkoba wake wa mkononi
pekee hali iliyoonesha hakuwa akienda mbali .
Walisema siku tatu baadaye walipatwa na
mshtuko mkubwa baada ya mlinzi wa hosteli
yao kuwaletea taarifa za kifo cha mwenzao
kilichotokea katika chumba cha mvulana
huyo anayeishi jirani .
MAJIRANI NAO WANENA
Majirani waliozungumza na gazeti hili
walisema kwao haikuwa mara ya kwanza
kumuona msichana huyo, kwani mara kwa
mara alikuwa akifika pale ingawa akishaingia
ndani hakuwa akitoka nje .
Walisema mara zote hizo , mwanaume huyo
mwenyeji ndiye alikuwa akitoka nje na
kwenda kumnunulia chakula .
Wananchi na wanausalama wakiwa eneo la
tukio .
POLISI WAUPELEKA MWILI HOSPITALI YA
TUMBI
Jeshi la polisi liliwasili eneo la tukio na
kuukuta mwili huo ukiwa umelala kitandani
ukiwa hauna jeraha , lakini pembeni yake
kulikutwa vidonge ambavyo havikufahamika
ni vya aina gani ambavyo pia vilichukuliwa
pamoja na mkoba wake hadi kituonis.
Minong ’ ono kutoka kwa majirani kuhusiana
na vidonge hivyo ilitofautiana , baadhi yao
walisema huenda vilitumika katika jaribio la
kutoa mimba , wengine walisema
inawezekana msichana huyo alipata ugonjwa
wa ghafla usiku na mwanaume huyo
alikwenda kumchukulia vidonge hivyo
ambavyo havikuweza kumsaidia marehemu
kupata nafuu .
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani , SACP
Ulrrich Matei alithibitisha kutokea kwa tukio
hilo na kusema juhudi za kumtafuta
mwanaume huyo zinaendelea huku madaktari
nao wakiendelea na uchunguzi wao ili kubaini
chanzo cha kifo hicho.
DENTI AFIA KWA HAWARA
7:54 AM
No comments
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment